Tuesday, 23 February 2016

Kocha Simba amtetea Kessy kuvurunda

KOCHA wa Simba Jakson Mayanja amemkingia kifua mchezaji wake Ramadhan Kessy kwa kile kinachodaiwa kuwa alifanya uzembe wa makusudi ulioigharimu timu yai
hadi kufungwa na Yanga mabao 2-0 kwenye Uwanja wa tTaifa Jumamosi.
Katika mchezo bao la kwanza lilisababishwa na makosa ya Kessy aliyekuwa akijaribu kumrudishia mpira kipa wake, Vincent Angban lakini ukawahiwa na Donald Ngoma na kufunga.
Baadhi ya mashabiki wamekuwa wakilalamika kuwa huenda Kessy aliuza mechi ndio maana alifanya uzembe wa makusudi, jambo ambalo Mayanja alisema kama ni makosa yalitendeka kwa wachezaji wote.
Akizungumza jana Dar es Salaam Mayanja alisema walijiandaa vizuri dhidi ya Yanga lakini kilichoshangaza wachezaji wake walicheza tofauti na kile walichoelekezwa.
“Hatuwezi kusema ni Kessy peke yake, wachezaji wote hawakucheza kama nilivyowaelekeza sijui ni nini kilitokea,”alisema na kuongeza kuwa watu wamekuwa wakilalamika bila kujua matatizo ya kiufundi.
Mayanja aliwashukuru mashabiki wa Simba kwa kuwaunga mkono katika mchezo huo huku pia akiwataka kutokata tamaa kwani kuna michezo mingine ya ligi inakuja.
Alisema kwa sasa anaangalia mbele michezo ijayo katika kuhakikisha inafanya vizuri kama ilivyotokea kwa michezo mingine.
Wakati Mayanja akiongea hayo, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga Jerry Muro alimpongeza Kocha huyo kwa kuwa muungwana.
Alisema Mayanja alionyesha uungwana kwa kuwa aliona kuwa wachezaji wake waliteleza na sio kumlaumu mwamuzi au mchezaji.

0 comments:

Post a Comment