BARAZA la Kilimo na Mifugo Tanzania (ACT), limempongeza Rais John
Magufuli kwa kuagiza vyombo vinavyohusika kusitisha uingizaji wa
sukari
kiholela nchini.
Kwa kuwa bado uzalishaji wa sukari nchini hautoshelezi mahitaji,
baraza hilo limeshauri kuwekwa mazingira mazuri ili wawekezaji waanzishe
mashamba mapya ya miwa na wakulima wadogo wawezeshwe kustawisha miwa
kwa tija.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari nchini Dar es
Salaam jana, baraza hilo limepongeza hatua hiyo ya Dk Magufuli ikiwemo
kusisitiza kwamba kama kuna upungufu, kujazia kwake kufanyike kwa
utaratibu ulio rasmi na wa wazi.
Ilisema katika kipindi cha nyuma, kutokana na uzalishaji sukari
kutotosheleza mahitaji, Serikali iliamua kutoa vibali kwa
wafanyabiashara kuingiza bidhaa nchini ili kufidia upungufu.
“Kwa bahati mbaya, baadhi ya watu waliopewa vibali, walivitumia
vibaya kwa maana ya kuagiza sukari nyingi zaidi ya mahitaji halisi. Kwa
kuwa nchi zinazozalisha sukari zinatoa ruzuku kwa wazalishaji, wanao
uwezo wa kupunguza bei bila kupata hasara. Hii ina maana kwamba
wanaozalisha sukari nchini, kamwe hawawezi kushindana na sukari
inayoagizwa kutoka nje,” ilisisitiza.
0 comments:
Post a Comment