Wednesday, 24 February 2016

Harmonize na Huddah, Roma Mkatoliki kuhusu kushoot video nje?

Kwenye 255 XXL Clouds fm leo, stori zilizopata airtime ni
pamoja na hii ya Harmonize  kueleza mahusianao yake na Huddah.
Harmonize


hapana bana mimi sitoki na Huddah ,  ni rafiki yangu alafu yupo hapa Dar kama siku nne amenitumia message  asubuhi akaniambia amefika nikamwambia karibu nikawa  niko busy sijaonana naye nilikuwa niko busy najiandaa kurelease wimbo’
‘Nikipata muda nitaenda kuwasiliana naye  kwasababu katoka kenya hajaja kwa ajili yangu pia ana mambo yake lakini pia akaona ni vizuri kuonana na mimi akatext akaniambia tuonane’
Unajua kazi ambayo Waziri Nape Nanauye alikuwa anapenda kufanya akiwa mtoto? ‘Mwanzo kabisa wakati ni nikisoma nilifikiria kuwa rubani wa ndege tena ndege za kijeshi sikutaka ndege za kawaida na ndo maana kwenye elimu yangu ya sekondari nilisoma sana masomo ya sayansi’ 
‘kwa bahati mbaya sikufanya vizuri somo moja kwahiyo nikashindwa kuendelea na hayo masomo nikaamua kusoma uchumi EGM, kama ni kazi nilitamani kufanya ni  kuwa rubani wa ndege lakini  badae nikapoteza hamu ya kufanya lakini nafikiri mbele ya safari kama wataniruhusu kurusha ndege za kawaida’
Baada ya wasanii kadhaa wa bongo kwenda kufanya kichupa nje ya nchi Roma Mkatoliki anazoplan za kwenda huko?
Mimi ninachoangalia ni wapi soko langu lipo, kwa mfano unaweza kwenda kushoot  ngoma mbele ukasema unataka kufanya international music lakini still unataka soko lako liwe Dar Live we nenda kashoot uko alafu unakuja na Roma Dar Live mimi najaza Dar Live kuliko wewe kwasababu mimi nilitagert pale
Roma Mkatoliki


0 comments:

Post a Comment