Friday, 22 April 2016

Video ya Mbunge Mwita Waitara kuhusu matangazo ya Bunge kuzuiliwa


April 19 2016 Bunge la 11 lilianza rasmi bungeni Dodoma, Baadhi ya Wizara zilianza kwa kuwasilisha bajeti zake na kutoa nafasi kwa washiriki kuzikubali au kuzikataa. Lakini moja ya tukio lililoonekana kuwa kikwazo kwa wengi na hata kulalamikiwa katika baadhi ya vyombo vya habari, ni hii ya kuzuiwa kwa Waandishi wa habari kurekodi baadhi ya matukio ndani ya bunge wakati vikao hivyo vikiendelea isipokuwa TBC pekee.
Hapa nakukutanisha na Mbunge wa Ukonga,  Mwita Waitara akizungumza kwenye Exclussive Interview na AYO TV ambapo anasema>>> ‘Kabla ya kuja bungeni tuliona taarifa ya kuwa TBC haitaonyesha vipindi vyote, bali itaonyesha kipindi cha maswali na majibu na vipindi vyenyewe vitarekodiwa na vyombo vingine vyote havitatakiwa kuingia na camera‘ ;-Mwita Waitara
Vyombo binafsi vinaweza kutoa taarifa kwa gharama zao, hawajaomba kulipwa na Bunge, kitendo kilichofanyika kuwazuia waandishi ni kitendo kibaya, huu ni uoga wa Serikali na nikuwaondoa watu katika utandawazi‘ ;-Mwita Waitara
Bunge limeelekezwa na Serikali na Serikali imeingilia uhuru wa unge, kwahiyo hili bunge hapa lilipo halina meno;-Mwita Waitara

0 comments:

Post a Comment