Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Kamishna Valentino Mlowola
Wakati
viongozi, wafanyabiashara na makampuni makubwa barani Afrika yakitajwa
kwenye kashfa ya ukwepaji kodi ya Panama papers, hapa nchini Taasisi ya
kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) imesema kuwa inafuatilia ripoti
hiyo kubaini kama kuna watanzania waliohusika.
Kashfa
hiyo ambayo had hivi sasa imekwisha tiskisa sehemu mbalimbali za dunia
inahusisha nyaraka zilizoibuliwa na mtandao wa waandishi wa habari
ambazo zinawafichua watu maarufu duniani wakiwamo wakuu wa nchi 12
walioko madarakani na waliostaafu pamoja na familia na rafiki zao wa
karibu ambao wamenufaika na ukwepaji kodi.
Wakati
nchi za watu maarufu kutoka barani Afrika kama Kenya, Afrika
Kusini,Nigeria, Zimbabwe, Angola, Congo na Rwanda zikitajwa kwenye
kashfa hiyo hakuna mtanzania wala kampuni ya hapa nchini inayohusishwa
na sakata hilo.
Lakini
Mkurugenzi wa Takukuru Kamishna Valentino Mlowola alifunguka kuwa
Taasisi yake bado inafuatilia kwa kina taarifa hiyo ili kujiridhisha
kama ni kweli hakuna Mtanzania yeyote anayehusika.
Alisema endapo itabainika kuwapo kwa watanzania kwenye kashfa hiyo watachukuliwa hatua kulingana na sheria zilizopo.
"Ninachoweza
kusema kwa sasa ni kwamba tunaendelea kuangalia ripoti na tukibaini
uwepo wa watanzania mambo mengine yatafuata ikiwa ni pamoja na
kuwachukulia hatua kulingana na sheria zetu za hapa nchini", alisema
Mlowola
0 comments:
Post a Comment